• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Orion yajitosa kwa biashara ya mtandaoni

Orion yajitosa kwa biashara ya mtandaoni

Na CHRIS ADUNGO

MADUKA ya Orion yanayofanya biashara ya mtandaoni humu nchini yamejiunga na shirika la ununuzi na uuzaji wa mitandaoni  humu nchini, Kenya Online Shopping Space, ambalo hivi karibuni limedhidhirisha kuwa mazingira ni shwari.

Biashara kupitia kwa intaneti (E-Commerce) huwezesha ununuzi na uuzaji wa bidhaa mbalimbali katika mitandao zikiwemo elektroniki, vyakula na mboga.

‘’Tunataka kutoa njia nyepesi inayowezesha  wateja kuagiza bidhaa na huduma kupitia mitandao,’’ akasema Peter Wangai,  mwasisi wa maduka ya mtandaoni ya Orion .

Sekta ya E-Commerce barani Afrika imekua kwa kasi na inatarajiwa kufika dola milioni 28,942 kufikia mwaka wa 2022 kulingana na ripoti  ya 2017 kuhusu mtazamo wa masoko ya dijitali.

‘’Tutatumia pia trafiki ya tovuti yetu kutangaza mapato tunayopata kutoka kwa washirika na watangazaji. Mwanzoni, Orion itafanya biashara kutokana na bidhaa zake ikishirikiana na wauzaji wa rejareja kwenye tovuti watakaolipwa kulingana na idadi ya bidhaa watakazouza.”

Kulingana na waujazi wa  mitandaoni, uuzaji wa rejareja wa mitandaoni umechukua asilimia 10 ya biashara hiyo kote duniani ambayo ina thamani ya dola trillion 290 kulingana na takwimu za mwaka wa 2017

Mwaka 2017,  kampuni ya Safaricom ya Kenya ilizindua biashara kwa njia ya intaneti iliyokuwa na bidhaa elfu ishirini kutoka kwa wachuuzi 160.

 

You can share this post!

Ni kujituma kulitusaidia, si ubunifu – Wenger

Conte akiri Chelsea kuingia Nne Bora ni ndoto

adminleo