• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Zoo yajifufua, Sofapaka yazikwa

Zoo yajifufua, Sofapaka yazikwa

Na CHRIS ADUNGO

TIMU ya Zoo Kericho Jumapili ilipata sababu ya kutabasamu baada ya kumaliza msururu wa kupoteza mechi ilipoizima Posta Rangers 1-0 katika uwanja wa Kericho.

Bao la pekee la mechi hiyo lilifungwa na Mike Madoya na kufuta matumaini ya vijana wa Sammy ‘Pamzo’ Omollo  kupata ushindi.

Sofapaka nao walipewa kichapo tena na Thika United. Kepha Aswani alipata bao la kwanza na kuwapa Batoto ba Mungu imani ya kupata pointi tatu lakini Mata Masakidi akasawazisha dakika chache baadaye.

Adem Edmond alihakikisha vijana wa Nicholas Muyoti wamepata ushindi wao wa kwanza msimu huu na kuwaacha vijana wa Sam Ssimbwa wakitafakari kuhsu mechi inayofuata.

Katika uwanja wa Bukhungu, Nakumatt iliendelea kurekodi matokeo duni baada ya kulimwa 2-0 na Kakamega Homeboyz.

You can share this post!

Conte akiri Chelsea kuingia Nne Bora ni ndoto

Ssimbwa ajiuzulu akilalamikia wachezaji kumgomea

adminleo