• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 1:29 PM
Mke wa mwanamume achukuliwa na mwenzake baada ya kupoteza ubashiri wa mechi

Mke wa mwanamume achukuliwa na mwenzake baada ya kupoteza ubashiri wa mechi

Na CHRIS ADUNGO

MWANAMUME mmoja atatazama kupoteza mkewe na kulala chumbani kwa rafiki yake wa kamari kwa wiki nzima baada ya kupoteza ubashiri wa mechi ya Man City dhidi ya Man United Jumamosi.

Kwenye makubaliano waliyoandikiana kwa mkono kwenye kijikaratasi, wanaume hao wawili kutoka Tanzania, kila mmoja aliapa kumpa mwenzake mkewe kwa muda wa wiki moja endapo angeshindwa kwenye utabiri wa matokeo ya mechi hiyo.

Ingawa Taifa Leo haiwezi kuthibitisha ukweli wa makubalino hayo yaliyosambazwa mitandaoni, mmoja wa wanaume hao sasa huenda akampoteza mkewe baada ya Man United kupigana kufa kupona na kuweza kuilaza Man City 3-2 katika mechi iliyochezwa uwanjani Etihad.

Makubaliano kati ya Amani Stanely na Shilla Tony kabla ya mechi ya debi ya Manchester. Picha/ Hisani

Katika kijikaratasi hiki hapa juu, Amani Stanley, ambaye ni shabiki sugu wa Man City, aliweka mkewe kama dhamana kabla ya timu yake kupigwa, huku mwezake Shilla Tony pia akikubali kupena mkewe Man United ingelimwa.

Ikiwa makubaliano haya yalikuwa ya kweli, basi utakuwa ni mfano wa hivi karibuni wa mashabiki sugu kusahau thamani ya pesa na badala yake kutumia wake zao kama dhamana katika ubashiri wa mechi.

 

 

You can share this post!

Wakenya wengi wanapenda simu za Tecno – Utafiti

Hali si shwari: Waiguru ayumbishwa na kimbunga cha siasa

adminleo