• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 6:50 AM
Pasta ashangaza kuomba waumini idhini afurushe mkewe

Pasta ashangaza kuomba waumini idhini afurushe mkewe

Na TOBBIE WEKESA

KABATI, MURANG’A

PASTA wa kanisa moja la hapa aliwaacha wengi vinywa wazi alipowaomba ruhusa waumini ili amtimue mke wake.

Inasemekana pasta alitangazia waumini masaibu aliyokuwa akipitia mikononi mwa mkewe na akawaomba ruhusa aweze kumfurusha.

Kulingana na mdokezi, pasta alichukua nusu saa kuelezea kanisa sababu za kufikia uamuzi huo. Kulingana na pasta, mkewe alikuwa mtu asiyeaminika  katika ndoa.

“Nikiondoka kwenda semina, mke wangu pia huondoka. Haendi kwao. Anakoenda mimi sijui,” pasta alieleza.

Kila mtu kanisani alikuwa ange kumsikia pasta. Wengi waliofahamu tabia  za mkewe walitabasamu. Penyenye zinasema mkewe alikuwa  akimcheza pasta  kwa muda mrefu.

Kila wakati pasta akiondoka nyumbani kwenda mikutano ya maombi, kipusa alikuwa akiondoka kwenda kwa mipango ya  kando.

Pasta alieleza namna alivyong’ang’ana na majukumu nyumbani hata mkewe akiwa.

“Ni Mungu tu amenitunza. Nimepitia mengi. Naomba idhini yenu ili nimtimue,” pasta alieleza.

Duru zinasema kabla ya kanisa kuanza, mwanadada huyo alikuwa amegundua mipango ya pasta. Aliamua kuondoka mapema akihofia kuaibishwa.

“Kama ni hayo unayopitia, pasta ruhusa tumekupa na utafute mwanadada mwingine atakayekutunza,” muumini mmoja alisimama na kumueleza pasta.

“Nimechoka kusikia hadithi mtaani. Jina langu limeharibika. Mke wangu hatulii. Sijui ameingiliwa na shetani gani,” pasta akasema.

Kulingana na mdokezi, waumini wote walikubaliana kwa kauli moja kumuunga pasta.

“Mfukuze. Tutakusaidia kupanga harusi nzuri. Huyo mke hata sisi tunajua mienendo yake,” muumini mmoja alisema kwa sauti huku wenzake wakikubaliana naye.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

MAKALA MAALUM: Wageukia magari ya serikali kusafirisha miti...

TAHARIRI: Magavana waelezane ukweli kwenye kongamano

adminleo