• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 3:17 PM
King’asti ampa Ronaldo ‘zawadi’ ya uchi wa mnyama

King’asti ampa Ronaldo ‘zawadi’ ya uchi wa mnyama

Na CHRIS ADUNGO

MWANAMITINDO maarufu mzawa wa Paraguay, Mirtha Sosa aliuduwaza ulimwengu wa soka kwa mara nyingine usiku wa Aprili 3, 2018 baada ya nyota Cristiano Ronaldo kufunga bao la Scorpion (nge) lililowachochea Real Madrid kuwabamiza Juventus 3-0 na hivyo kuwabandua miamba hao wa soka ya Italia kwenye robo-fainali za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu.

Mirtha, ambaye anaaminika kuwa shabiki mrembo zaidi wa Real kuwahi kutokea nchini Paraguay, si mgeni wa kusalia uchi wa mnyama kila wakati Ronaldo anapowatambisha waajiri wake ndani na nje ya uwanja wa Santiago Bernabeu.

Akipania kumtia fowadi huyo mzawa wa Ureno kishawishini mapema wiki iliyopita, Mirtha alivua nguo zote na kutembea tupu katika hatua aliyoitaja kuwa ‘zawadi’ maridhawa na mahsusi kwa Ronaldo ambaye kwa sasa anatoka kimapenzi na kipusa Rhian Sugden, 31, anayetishia kuichukuwa nafasi ya Georgina Rodriguez aliyemzalia mwansoka huyo mtoto Alana Martina mwishoni mwa mwaka jana.

Akiwa fundi wa masuala ya ngono na gwiji wa kuvua nguo kwa lengo la kuwataka wanasoka wenye mishahara minono kuvutiwa na ukubwa wa makalio yake, Mirtha aliwahi pia kusalia uchi wa mnyama baada ya Ronaldo kutawazwa Mchezaji Bora Duniani mwishoni mwa 2017.

Wiki iliyopita, kichuna huyo alipakia tena picha za uzushi kwenye mitandao yake ya kijamii kwa kusherehekea ushindi Real na ufanisi wa Ronaldo kwa upekee aliouzoea. Kwenye mojawapo ya picha, Mirtha mwenye umri wa miaka 32 alionekana kuandika makalioni nambari saba kuashiria jezi anayoivalia Ronaldo kambini mwa Real na katika timu ya taifa ya Ureno.

“Ni picha mahsusi kwa Ronaldo ambaye penzi lake linachoma na kunitesa! Hongera kwa ufanisi wako mpenzi! Mashabiki lisheni macho, ila jueni mzinga mzima unamsubiri Ronaldo ambaye namtaka aache mwendo wa kobe; afanye hima aje ajirinie asali kiasi chake,” akaandika kidosho huyo aliye na takriban wafuasi 480,000 kwenye mtandao wa Instagram.

Isitoshe, Mirtha alitangaza kuwa kwa sasa yeye ni mtani na mpinzani rasmi wa mwanamitindo mzawa wa Brazil, Suzy Cortez, 26, ambaye pia amekuwa na mazoea ya kuvua nguo na kutumia ukubwa wa ghuba zake kuwatia kishawishini nyota wa Barcelona – Lionel Messi, Philippe Coutinho na Gerard Pique. Suzy alitawazwa mshindi wa Miss BumBum mnamo 2015 nchini Brazil.

“Sawa na Suzy ambaye amefunguka kuhusu jinsi anavyoliwania penzi la baadhi ya wanasoka maarufu wa Barcelona, nami sioni nikimnyima Ronaldo tunda hili iwapo ataomba kulionja!” akasema Mirtha ambaye amekuwa akisafiri mbali na karibu kwa minajili ya kumshangilia Ronaldo kila anaposhuka dimbani kuongoza mashambulizi ya Real.

 

 

You can share this post!

TAHARIRI: Magavana waelezane ukweli kwenye kongamano

ADUNGO: Chini ya Klopp, Liverpool inaweza kufanya lolote...

adminleo