• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 5:55 AM
Buda afumania mkewe peupe akigawa asali sebuleni

Buda afumania mkewe peupe akigawa asali sebuleni

Na BENSON MATHEKA

EMBAKASI, NAIROBI

KALAMENI wa hapa hakuamini macho yake alipompata mkewe akigawa asali kwenye kochi katika sebule ya nyumba yake.

Inasemekana badala ya kuaibika baada ya kufumaniwa, mwanamke huyo ambaye ni mama ya watoto wawili wanaosomea shule za mabweni alimkabili mumewe na kumlaumu kwa kutomkata kiu ya uroda.

Kulingana na mdokezi wetu, jamaa ambaye ni afisa katika shirika moja la kiserikali, alikuwa na tabia ya kutumia muda wake vilabuni akipiga soga na marafiki na mkewe alikuwa akidai kwamba akifika nyumbani alikuwa akilala fofofo.

“Mkewe aliamua kutafuta mwanamume wa kumtimizia mahitaji yake ya uroda. Alidai kuwa mumewe alikuwa ameshindwa na majukumu yake ya unyumba na akafaulu kumpata jamaa ambaye alikuwa akimwalika nyumbani mumewe akiondoka,” alieleza mdokezi.

Siku ya kisanga,  mumewe aliondoka kwenda kazini lakini  wakubwa wake wakamweleza alitakiwa kwenda nje ya nchi jioni kwa ziara ya kikazi.

Walimwambia arudi nyumbani kujiandaa kusafiri jioni hiyo. Ni alipofika nyumbani alipompata mkewe akiendelea kurushana roho na mpango wake wa kando.

Kulingana na mdokezi, hata kabla ya kalameni kutamka lolote, mkewe alimkabili kwa maneno huku jamaa aliyefumaniwa akiramba asali ya mwenyewe akitulia.

“Usijaribu kumguza huyu jamaa.  Umeshindwa na kazi na  ni mimi niliyemwalika hapa kunishughulikia. Unafaa kuniuliza mimi kama una la kusema,” mama alimwambia mumewe.

Kalameni alihema kwa hasira, chozi likamtoka, kisha akamweleza mkewe kwamba amempa ruhusa ya kuendeleza nderemo zake na jamaa huyo.

Hata hivyo, aliwaambia hiyo ilikuwa siku ya mwisho kutumia nyumba yake kama danguro.

Alimsimamia mkewe akakusanya virago vyake kisha akaondoka na jamaa huyo na haikujulikana kilichojiri baada ya jamaa kurejea kutoka ziara ya kazi.

…WAZO BONZO…

 

You can share this post!

Walimu wanaochochea wanafunzi kugoma waonywa

Jeshi laokoa wanawake 54 na watoto 95 kutoka Boko Haram

adminleo