• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 7:55 PM
Sofapaka yamtimua Waliaula baada ya Ssimbwa kujiuzulu

Sofapaka yamtimua Waliaula baada ya Ssimbwa kujiuzulu

Na CHRIS ADUNGO

SIKU moja baada ya kocha mkuu Sam Ssimbwa kujiuzulu, Sofapaka Jumanne imempiga kalamu meneja wa timu hiyo Willis Waliaula.

Afisa wa klabu hiyo aliyesema na Goal.com alithibitisha taarifa hizo akisema: “Ndiyo, Waliaula si meneja wetu tena. Nafasi yake kwa sasa imetwaliwa na Hillary Echesa.”

“Ni uamuzi ambao ulifikiwa na usimamizi wa timu ili kuleta amani na maelewano kwa timu. Kumekuwa na  migogoro baina ya benchi la kiufundi na wachezaji.”

“John Baraza atasalia kuwa kocha wetu mkuu kwa sasa, lakini mipango ipo kumleta kocha mwenye uzoefu na tajriba katika soka.”

Batoto ba Mungu kwa sasa wako katika nafasi ya nne ligini wakiwa na pointi 16.

You can share this post!

ONYANGO: Isiwe mabasi ya NYS ni ya kunufaisha watu fulani

Klopp amfunza Guardiola gozi la UEFA

adminleo