• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 9:12 AM
Juventus yakabiliana na Real Madrid baada ya penalti chungu

Juventus yakabiliana na Real Madrid baada ya penalti chungu

Na CHRIS ADUNGO

TIMU ya Juventus Jumatano usiku ililazimika kuaga kipute cha Klabu Bingwa Ulaya baada ya refa kuipa Real Madrid penalti katika muda wa ziada.

Juventus tayari ilikuwa ishafunga mabao matatu ugenini Santiago na kusawazisha matokeo ya jumla kuwa 3-3  huku uwezekano wa muda wa ziada wa dakika 30 ukiwepo.

Lakini Medhi Benatia wa Juventus alionekana kumwangusha Lucas Vazquez ndani ya kisanduku baada ya kupokea pasi kwa kichwa kutoka kwa Cristiano Ronaldo.

Refa wa Uingereza Michael Oliver alizungukwa na wachezaji wa Juventus huku akimpa kadi nyekundu kipa Gianluigi Buffon hata kabla ya penalti kupigwa.

Ronaldo aliutia mpira ndani ya neti na kuiwezesha Real Madrid kufika nusu fainali kwa ujumla wa mabao 4-3.

Matokeo hayo yaliwaletea uchungu mwingi wachezaji wa Juventus na mashabiki kote duniani.

Baada ya mechi wachezaji wa Juventus waliwakabili wenzao wa Real wakighadhabishwa na uamuzi wa kuwabandua kwa shindano hilo, lakini Sergio Ramos alikuwepo kujaribu kutuliza hali.

Haijulikani iwapo UEFA itamchukulia hatua Ramos kwa kujitokeza baada ya mechi, ikizingatiwa alikuwa ashpigwa marufuku katika mechi hiyo.

 

You can share this post!

KCB yatuza kikosi cha voliboli

Buffon: Michael Oliver ana jaa la taka rohoni, alifaa kula...

adminleo