• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 6:55 AM
De Bruyne akiri mpinzani Salah ni moto wa kuotea mbali

De Bruyne akiri mpinzani Salah ni moto wa kuotea mbali

Na AFP

KIUNGO mahiri, Kevin De Bruyne wa Manchester City amekubali kwamba mpinzani wake mkuu kwa vita vya Mchezaji Bora wa Mwaka EPL, Mohamed Salah ni moto wa kuotea mbali.

Habari zaidi zimesema kwamba Mbelgiji huyo amempigia kura Salah kumtaka ashinde tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Salah ameibukia kuwa mkali kutokana na ubora wake katika mechi za EPL na michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya.

De Bruyne amekuwa akipewa nafasi kubwa ya kutwaa tuzo hiyo kutokana na mchango wake katika kikosi cha Pep Guardiola kuelekea ushindi wa ligi ya EPL.

Lakini Salah aliyetwaliwa na Liverpool akitokea AS Roma ameonekana kuwa tishio baada ya kufunga mabao 29, hata baada ya kutokuwa kikosini mwishoni mwa wiki dhidi ya Everton.

Nyota mwingine aliye kwenye vita vya kuwania tuzo hiyo ni Harry Kane wa Tottenham.

 

You can share this post!

Serikali itangaze kansa janga la kitaifa – Wabunge

Sekta za elimu na afya kufaidi pakubwa kwa bajeti ya ziada

adminleo