• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Ajitia kitanzi akilalamikia kuchoshwa na mkewe

Ajitia kitanzi akilalamikia kuchoshwa na mkewe

BARACK ODUOR na CHARLES WASONGA

MWANAMUME mmoja katika kaunti ya Homa Bay Alhamisi alijiua katika mti wa maembe kwa madai kuwa alikuwa “amechoshwa” na mkewe.

Kisa hicho kilitokea katika kijiji cha Kowuor, kaunti ndogo ya Rachuonyo Mashariki.

Chifu wa eneo hilo Kennedy Otieno alisema kuwa mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 30 alijua kwa kamba ya mkonge nyumbani kwake baada ya kumtumia dadake ujumbe mfupi akimwambia kuwa “nimechoshwa na mke wangu.”

Kulingana na chifu huyo mwanamume huyo hakufafanua sababu iliyopelekea yeye kusinywa na mkewe kiasi cha kujinyonga.

Kamanda wa Polisi kaunti ya Homa Baye Marius Tume alithibitisha kisa hicho na kusema kuwa maafisa wake wameanzisha uchunguzi kuhusiana na kifo hicho.

Mwili wa marehemu umepelekwa katika Hifadhi ya Maiti ya Hospitali ya Rachuonyo Kusini kufanyiwa upasuaji.

 

You can share this post!

Huenda bei ya bidhaa ikashuka baada ya hatua hii

Mbunge ataka siasa za 2022 zikomeshwe

adminleo