• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Kenya yalazimishwa sare tasa na Ethiopia U-17

Kenya yalazimishwa sare tasa na Ethiopia U-17

Na GEOFFREY ANENE

KENYA imeambulia sare tasa dhidi ya Ethiopia katika mechi yake ya pili kwenye mashindano ya soka ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 yaliyoingia siku yake ya nne nchini Burundi hapo Aprili 17, 2018.

Vijana wa kocha Michael Amenga walitafuta ushindi bila mafanikio. Ushindi ungewapa Wakenya tiketi ya kushiriki nusu-fainali wakiwa bado wanasalia na mechi moja ya Kundi A dhidi ya Somalia hapo Ijumaa.

Kenya ilianza kampeni kwa kunyuka Burundi 4-0 Aprili 14 nayo Somalia ilipata alama tatu na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Ethiopia katika mechi yake ya ufunguzi Aprili 15.

Ethiopia ndiyo ilishinda Somalia uwanjani 3-1, lakini ikakonywa alama hizo baada ya kupatikana na hatia ya kuchezesha wachezaji watatu waliozidi umri wa miaka 17. Burundi na Somalia zilipangiwa kumenyana katika meci nyingine Aprili 17.

Kikosi cha Kenya: Wachezaji 11 wa kwanza – Maxwell Mulili (kipa), Lawrence Otieno, Telvin Maina, Christopher Raila, Arnold Onyango, Nicholas Omondi, Patrick Ngunyi, Hillary Okoth, Isaiah Abwal, Lesley Otieno, Mathew Mwendwa.

Wachezaji wa akiba – Brian Olango, Costah Anjeo, Nesta Wangema, Michael Abongo, Felix Chabaya, Daniel Ochieng, Said Musa.

You can share this post!

Pigo kwa Gor Tuyisenge kukosa stakabadhi za kusafiri Afrika...

Kesi 5 za wizi benki ya Equity kuunganishwa

adminleo