• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Wabunge wa Ruto Mlima Kenya wakaangwa mitandaoni

Wabunge wa Ruto Mlima Kenya wakaangwa mitandaoni

Katuni ya kejeli iliyotundikwa mitandaoni Alhamisi. Grafiki/ Peter MBuru

NA PETER MBURU

JUHUDI  za wabunge wanne kutoka eneo la Mlima Kenya kumpigia debe Naibu Rais William Ruto licha ya upinzani mkali wa kisiasa unaomkosesha usingizi zimewazolea kejeli na ucheshi miongoni mwa Wakenya, japo wengi wakizichukulia kuwa mzaha tu.

Wabunge hao wakiongozwa na Moses Kuria (Gatundu Kusini), Kimani Ichungwa (Kikuyu), Rigathi Gachagua(Mathira) na Ndindi Nyoro (Kiharu) wamekuwa wakizunguka maeneo mengi nchini wakieneza ajenda ya ubora wa Bw Ruto kuwa rais ifikapo 2022.

Na licha ya viongozi wengi kutoka eneo la Mlima Kenya kupunguza kasi lifikapo suala la kumpigia debe Naibu wa rais, huku wengine wakionyesha dalili za kumtema, wanne hao wamesalia dhabiti kumuunga mkono.

Katuni ya grafiki yaonyesha Bw Ruto akiondolewa uchovu na wabunge wa Mlima Kenya. Grafiki/ Peter Mburu

Ni hali hiyo ambayo imewafanya Wakenya kuchangamkia suala hilo na kueleza wanavyohisi katika mitandao ya kijamii, japo wakitumia njia za ucheshi zinazooashiria kuwa huenda wabunge hao wanampotosha Bw Ruto.

Picha za vibonzo vya viongozi hao zimekuwa zikisambaa kuashiria viongozi wasio na mashiko na ambao naibu wa rais ameaminia kumzolea kura kutoka eneo ambalo uwezekano wa kumtenga hauwezi kuepukika.

Nao viongozi hao wameshikilia ishara yao ya kikazi kuhakikisha kuwa wanauza ajenda za Bw Ruto kila wanapokanyaga, hata kama wanaouzia hawasikii wala kukubali.

Bw Kuria ambaye ndiye kigogo hapo amekuwa akitembea hata sehemu zilizo ngome za upinzani na kuwataka kumuunga mkono Bw Ruto.

Wabunge wenzake nao wamekuwa wakionekana katika mikutano ya Naibu wa rais mara kwa mara.

You can share this post!

KAULI YA WALIBORA: Namshukuru Jagina Shamte kwa sahihisho...

Katibu adai hongo ya Sh5 milioni katika zabuni ya maharagwe

adminleo