• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 8:50 AM
Tumia muafaka kunirejesha Kenya, Miguna amlilia Raila

Tumia muafaka kunirejesha Kenya, Miguna amlilia Raila

Na WYCLIFFE MUIA

WAKILI Miguna Miguna sasa anamtaka kinara wa ODM Raila Odinga kutumia muafaka aliyotia saini na Rais Uhuru Kenyatta kumrudisha humu nchini ili kudhihirishia Wakenya kuwa analenga kuleta umoja.

La sivyo, Bw Miguna anamtaka Bw Odinga kuelezea Wakenya kwa nini muafaka wake na Rais Kenyatta haujamuwezesha kurejea nchini kutoka Canada licha ya kuwaahidi kuwa atahakikisha amerejea.

Mnamo Machi 9, Bw Odinga na Rais Kenyatta waliafikiana kufanya kazi pamoja lakini siku chache baadaye Bw Miguna akafurushwa hadi Canada na serikali ya Kenya kuhusiana na utata wa uraia wake.

“Kama nilituhumiwa kwa kukuapisha, kwa nini haukukamatwa na kufurushwa kutoka Kenya kama mimi…? Kama salamu zako na Uhuru zinalenga kuunganisha nchi, kwa nini sijarudishwa Kenya? Elezea Wakenya wazi wazi,” Miguna alimwambia Bw Odinga kupitia mtandao wake wa Twitter.

 

You can share this post!

MAKALA MAALUM: Abubakar, kakake Joho, ndiye Sultan kamili...

Maafisa watofautiana kuhusu kafyu ya arusi

adminleo