• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Tanzania watwaa ubingwa Cecafa U-17 baada ya kuilima Somalia

Tanzania watwaa ubingwa Cecafa U-17 baada ya kuilima Somalia

Na GEOFFREY ANENE

TANZANIA ndiyo mabingwa wa makala ya tatu ya mashindano ya soka ya Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) ya Under-17 yaliyokamilika nchini Burundi hapo Aprili 29, 2018.

Serengeti Boys ilinyuka Somalia 1-0 katika fainali ngumu na kusisimua uwanjani Ngozi nchini Burundi.

Watanzania walipata bao la ushindi kupitia Edson Jeremiah katika dakika ya 25.

Mabingwa wa mwaka 2009 Uganda walishinda medali ya shaba kwa kutitiga Kenya 4-1 uwanjani humu Aprili 28.

Mabingwa wa mwaka 2007 Burundi pamoja na Ethiopia na Sudan walibanduliwa nje katika mechi za makundi.

Zanzibar ilifurushwa kutoka mashindano haya baada ya kuwasili nchini Burundi na wachezaji 12 walipitisha umri wa miaka 17.

Ethiopia ilipigwa faini ya Sh500, 252 kwa kuchezesha wachezaji watatu waliozidi umri wa miaka 17 katika mechi ya ufunguzi dhidi ya Somalia na kupokonywa ushindi waliokuwa wameandikisha wa 3-1. Somalia ilitunukiwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Ethiopia. Zanzibar ilipigwa marufuku kushiriki mashindano yoyote ya Cecafa hadi ilipe faini ya Sh1, 500,757 kutokana na udanganyifu huo.

You can share this post!

Gor yaibwaga Ingwe kuchuana na Hull City Mei 13

‘YouTube Man’ alenga kufufua makali yake...

adminleo