• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:55 AM
Rais Kenyatta namba wani Afrika kwa miundomsingi

Rais Kenyatta namba wani Afrika kwa miundomsingi

Na BERNARDINE MUTANU

RAIS Uhuru Kenyatta ametangazwa mshindi wa mwaka huu Afrika katika tuzo za uchukuzi na mifumo ya barabara.

Katika hafla iliyofanywa jijini Dakar, Senegal Jumamosi, shirika la Africa Road Builders lilimtangaza Rais Kenyatta kuwa mshindi wa tuzo ya Babacar Ndiaye 2018, kwa kuanzisha miradi katika mfumo wa uchukuzi wa reli, barabara pamoja na uchukuzi wa ndege.

Rais wa Habari, Miundo Msingi na Fedha Barani Afrika Adama Wade alitaja reli ya kisasa (SGR) kati ya Nairobi na Mombasa kuwa mradi muhimu sana ambao ulikuwa na manufaa makubwa kwa wananchi.

“Mradi wa SGR umepunguza nauli kati ya Nairobi na Mombasa kwa nusu na pia muda unaotumiwa kusafiri kati ya miji hii umepungua sana,” alisema.

Mradi huo ulilenga uchukuzi wa abiria milioni moja kwa mwaka. Pia serikali ililenga kupunguza msongamano katika barabara kuu za humu nchini.

Kwa kumpongeza Rais Kenyatta, kamati ya uteuzi wa washindi ilitangaza kuwa tuzo hiyo itatolewa Mei 23, mjini Busan, Korea Kusini, wakati wa mkutano mkuu wa kila mwaka wa Benki ya African Development.

 

You can share this post!

Wandani wa Raila wamshauri ajitose debeni 2022

Magavana 10 sasa walenga urais na useneta 2022

adminleo