• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 2:16 PM
Mipango yangu yote ya kando ni Wakikuyu – Sonko

Mipango yangu yote ya kando ni Wakikuyu – Sonko

Na CAROLYNE AGOSA

GAVANA wa Nairobi Mike Sonko alizua kicheko baada ya kusisitiza kuwa hana kinyongo na jamii ya Wakikuyu na kufichua kuwa hata ‘mipango wake wote wa kando’ wanatoka jamii hiyo.

Kwenye kanda ya video iliyosambazwa katika mtandao wa kijamii wa Twitter, Gavana Sonko alitaja nyadhifa mbalimbali za juu katika serikali yake ambazo ameteua Wakikuyu.

“Watu walisema Sonko hapendi Wakikuyu. Mimi ningependa kusema napenda Wakikuyu. Nimeteua madiwani Wakikuyu zaidi ya 10. Naibu gavana (wa Nairobi) anayekuja ni mwanamke Mkikuyu. Katibu wangu wa kaunti ni Mkikuyu. Baraza langu lina mawaziri wanne Wakikuyu.

Mkuu wa watumishi wangu ni Mkikuyu. Niko na maafisa wakuu sita wa idara ambao pia ni Wakikuyu,” alisema Bw Sonko.

Gavana huyu wa Nairobi, ambaye anatoka jamii ya Wakamba, aliibua kicheko katika umati alipoeleza uhusiano wake wa kifamilia na Wakikuyu.

“Wake wangu wa kwanza ni Wakikuyu. Watoto wangu ni Wakikuyu. Wakwe zangu ni Wakikuyu. Mipango yangu ya kando wote ni Wakikuyu!”

Kanda hiyo inakujia wiki chache baada ya Gavana Sonko kukemea kundi la wanasiasa na viongozi fulani aliodai wanajizatiti kumfanya aonekane ni kizingiti kwa maslahi ya jamii ya Wakikuyu – ambao wanadhibiti biashara nyingi jijini Nairobi.

Bw Sonko alipuuza madai kuwa analenga jamii hiyo katika msururu wa hatua za kuwafuta kazi wafanyakazi wa baraza la jiji, akisema nia yake ni kuwang’oa wafisadi na mabwanyenye ambao wameliteka jiji.

“Niko na watu kutoka jamii ya Kikuyu walio na vyeo vya juu katika serikali yangu. Mtu asieneze uvumi wa uongo kwamba nimewatenga (Wakikuyu),” akasema katika hafla moja City Hall mwezi jana.

You can share this post!

Miguna aapa kurejea nchini hapo Mei 16

ODM kupigania fidia kwa jamii zote zilizopoteza jamaa

adminleo