• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 10:21 AM
Aliyefanyiwa upasuaji vibaya akijifungua Gatundu afariki

Aliyefanyiwa upasuaji vibaya akijifungua Gatundu afariki

Na LAWRENCE ONGARO

MWANAMKE aliyefanyiwa upasuaji vibaya alipokuwa akijifungua katika hospitali ya Gatundu Level 4 wiki mbili zilizopita, alifariki wikendi.

Mama huyo wa miaka 30 alikuwa ameenda katika hospitali hiyo alipopatwa na uchungu wa uzazi na akazaa mtoto wa kiume kupitia upasuaji.

Kulingana na nduguye, Bw Mwangi Kanyingi, siku tatu baada ya kurejea nyumbani, alihisi maumivu makali tumboni na akarejeshwa katika hopsitali hiyo, lakini madaktari wakapendekeza apelekwe Thika Level 5 kwa matibabu zaidi.

“Sisi kama familia tulimpeleka tena hadi Thika ili afanyiwe uchunguzi zaidi. Baadaye alilazwa huko kwa mara nyingine, huku madaktari wakipendekeza afanyiwe  upasuaji mara nyingine ili kubaini tatizo. Baada ya upasuaji huo wa pili, alivuja damu nyingi na kuaga dunia,” alisema Bw Kanyingi.

Waziri wa Afya  katika Kaunti ya Kiambu, Dkt Joseph Murega alisema wanachunguza chanzo cha marehemu kuvuja damu nyingi.

“Tayari tumewasilisha chembe chembe za damu yake katika mahabara  ya serikali jijini Nairobi ili ifanyiwe uchunguzi zaidi kubainisha sukweli wa mambo,” alisema Dkt Murega.

 

You can share this post!

Mvua zaidi yaja, Idara ya Utabiri yasema

OBARA: Serikali isibadili sembe bila ruhusa ya raia wake

adminleo