• Nairobi
  • Last Updated March 18th, 2024 8:55 PM
Jaji Ouko awataka wenzake kujiepusha na ufisadi

Jaji Ouko awataka wenzake kujiepusha na ufisadi

Na RICHARD MUNGUTI

Rais wa Mahakama ya Rufaa Jaji William Ouko Jumanne aliwahimiza majaji watumie uhuru waliopewa katiba kwa manufaa ya umma.

Jaji Ouko aliwataka majaji wote wawe wakizingatia haki za umma wanapotekeleza majukumu yao.

Jaji Lydia Achode alipoapishwa kuwa Jaji msimamizi wa Mahakama Kuu Mei 15, 2018. Picha/ Richard Munguti

Akizugumza wakati wa kuteuliwa kwa Jaji Lydia Achode kuwa Jaji msimamizi wa Mahakama kuu, Jaji Ouko alisema Rais Uhuru Kenyatta aliitaka idara ya mahakama ishiriki katika utekelezaji wa Ajenda Nne Kuu za Serikali ambazo ni Afya, Uzalishaji wa vyakula vya kutosha , utengenezaji bidhaa viwandani na makao bora.

Jaji huyo aliwahimiza majaji na mahakimu wachukulie kazi zao kwa uzito na kujiepusha na visa vya ufisadi.

“Kama vile Rais Kenyatta alisema  nawahimiza majaji na mahakimu msikilize na kuamua kesi za ufisadi kwa wakati unaofaa ndipo matajiri na mabwanyenye wasichukulie maagizo ya korti kwa mzaha,” alisema Jaji Ouko.

You can share this post!

Washukiwa wengine 3 wakodolea macho kifo

Pasta akana kuvamia shamba Kariobangi

adminleo