• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 3:34 PM
Bomba jipya la KPC kusafirisha lita milioni 1 kwa saa

Bomba jipya la KPC kusafirisha lita milioni 1 kwa saa

Na BERNARDINE MUTANU

Mafuta ya kwanza yaliyoboreshwa yataanza kusafirishwa kwa kutumia bomba mpya la mafuta Julai 1.

Bomba hilo limetengenezwa kwa gharama ya Sh48 bilioni. Kampuni ya Kenya Pipeline ilisema ilimaliza kutengeneza mfumo wake na kuunganisha na umeme mnamo Machi 2018.

Bomba hilo lina uwezo wa kupitisha 2.6 milioni za mafuta kwa lisali moja kutoka Mombasa hadi Nairobi.

Julai 1, lita milioni moja kwa saa moja zitasafarishwa kwa kutumia bomba hilo. Lina kipenyo cha inchi 20 na litakuwa na uwezo wa kutosheleza Kenya na majirani wake mahitaji ya mafuta mpaka 2044, alisema meneja Mkurugenzi wa KPC Joe sang.

“Tunatumia teknolojia mpya ili kurahisisha uchukuzi wa mafuta na bidhaa zingine zinazotokana na petroli.

KPC pia imesakini pambu nne mpya maeneo ya Changamwe, Maungu, Mtito Andei na Sultan Hamud na pampu zingine za kuimarisha operesheni katika eneo la Kipevu.

You can share this post!

Ni faida tu kwa benki ya Equity

ERC inavyowaumiza watumizi wa mafuta taa

adminleo