• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 8:55 AM
Washukiwa wa mauaji wamtisha kiongozi wa mashtaka

Washukiwa wa mauaji wamtisha kiongozi wa mashtaka

Na RICHARD MUNGUTI

HAKIMU mwandamizi Bi Martha Mutuku alimtaka kiongozi wa mashtaka Bw Solomon Naulikha atayarishe ushahidi wote katika kesi ambapo washukiwa watano wanakabiliwa na mashtaka ya wizi wa mabavu.

Miongoni mwa walionyang’anywa na kuuawa ni aliyekuwa Rubani wa Shirika la Ndege la Kenya Airways Bw Ng’ang’a.

Baada ya kumuua washukiwa hao walidaiwa walificha maiti yake kwa shimo la choo.

Bi Mutuku alimwagiza Bw Naulikha awasiliane na maafisa wawasiliane na maafisa wa polisi wanaochunguza kesi hiyo na kuwapa washukiwa nakala za mashahidi.

Hakimu alitoa agizo hilo baada ya washtakiwa kumlalamikia wamekuwa wakiteswa na polisi kwa kutopewa nakala za mashahidi.

“Naomba hii mahakama iamuru  afisa anayechunguza kesi hii, polisi na Bw Naulikha wajiandae sawasawa kwa vile kutakuwa na kivumbi kesi hii ikianza,” alisema mmoja washtakiwa Bw Daniel Kioko.

Bw Kioko alisema polisi wamekuwa wakichukulia kesi hiyo kwa mzaha ila hawajui “maisha yao (washtakiwa) yamo hatarini.”

Watano hawa wakiongozwa na Bw Daniel Kioko walimlalamikia Bi Mutuku kwamba maafisa wa polisi wanaochunguza kesi hii wanawachezea kwa kutowapa nakala za mashahidi.

Watano hao walimtaka Bw Naulikha ajiandae kwa vile siku ya kusikizwa kwa kesi “atajua kilichomtoa kanga manyoya na kile kinasababisha nyani kuishi juu ya miti.”

Kesi itasikizwa Julai 23, 2018.

You can share this post!

Watu 8 washtakiwa kunyang’anya Muriuki Sh100,000

Timu za Kenya na TZ kuwania ubingwa wa SportPesa Super Cup

adminleo