• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
VITUKO UGHAIBUNI: Mwislamu aliyeua ng’ombe auawa na umati

VITUKO UGHAIBUNI: Mwislamu aliyeua ng’ombe auawa na umati

Na AFP na VALENTINE OBARA

NEW DELHI, INDIA

MWANAMUME Mwislamu aliyekashifiwa kwa kuua ng’ombe alipigwa hadi kufariki na umati katika eneo la kati mwa India, polisi walisema Jumapili.

Tukio hilo limeongeza idadi ya mauaji yanayotendwa na halaiki dhidi ya watu wanaochinja wanyama ambao huabudiwa na Wahindi.

Siraj Khan ambaye alikuwa mshonaji nguo mwenye umri wa miaka 45, alishambuliwa katika Wilaya ya Satna iliyo Jimbo la Madhya Pradesh mapema Ijumaa iliyopita, akafariki papo hapo, kwa mujibu wa afisa wa polisi wa eneo hilo Arvind Tiwari.

Rafiki yake, Shakeel Maqbool, ambaye pia alishambuliwa, alilazwa hospitalini akiwa katika hali mahututi.

Polisi karibu 400 walipelekwa eneo hilo Jumamosi kuendeleza uchunguzi, kulingana na gazeti la Press Trust of India.

“Tumekamata watu wane, na wameekwa kizuizini. Tunachunguza kilichosababisha shambulio hilo,” akasema Tiwari.

Aliongeza kuwa polisi walipata nyama na mzoga wa beberu katika eneo la mkasa lakini hakutoa maelezi zaidi kwani uchunguzi ungali uanendelea.

Wahindi huchukulia ng’ombe kama viumbe vitakatifu na ni hatia kuchinja au kupatikana au kula nyama ya ng’ombe katika majimbo mengi nchini humo.

Uchinjaji wa ng’ombe katika Jimbo la Madhya Pradesh hupokea adhabu ya kifungo cha miaka isiyozidi saba gerezani lakini katika majimbo mengi India adhabu ya kisheria huwa ni kifungo cha maisha gerezani.

You can share this post!

VITUKO UGHAIBUNI: Mtoto wa miujiza azaliwa katika kisiwa...

VITUKO UGHAIBUNI: Mwanamume huyu hulipa Sh292,000 kunyolewa

adminleo