• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 PM
Nilijua tungeinyorosha Ulinzi Stars, asema kocha Baraza

Nilijua tungeinyorosha Ulinzi Stars, asema kocha Baraza

Na CHRIS ADUNGO

KOCHA wa Sofapaka, John Baraza amesema alikuwa na hakika kuwa timu yake ingeizaba Ulinzi Stas wikendi.

Mabao kutoka kwa Umaru Kasumba na Kepha Aswani yalifuta bao la Elvis Nandwa la kufuta machozi, huku mabingwa hao wa ligi 2009 wakiwafikia Ulinzi kwa pointi.

Kocha huyo anatumai ushindi huo utasaidia vijana wake kuandikisha matokeo bora zaidi katika meci zijazo, huku ubingwa bado ukiwa kiganjani.

“Motisha ilikuwa juu kabla ya mechi, wachezaji waliahidi wangefanya makubwa na hawakufeli. Tulijua tungewanyorosha na nina furaha tuliwazima. Wiki hiyo imekuwa nzuri kwetu, tulifanya mazoezi ya kutosha na nafurahi mbinu zetu zilileta matokeo mema.

“Kwa sasa tunaangazia mechi zijazo tukilenga kuzoa alama za juu zaidi,” aaksema Baraza.

Kufikia sasa, Batoto ba Mungu wako katika nafasi ya tatu kwa jedwali wakiwa na pointi 17.

You can share this post!

Straika wa Nzoia atwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Aprili

Raila ajiandaa kustaafu siasa

adminleo