• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 5:41 PM
Wezi wa ng’ombe wauawa na umma wakiiba nyati

Wezi wa ng’ombe wauawa na umma wakiiba nyati

Na GEOFFREY ANENE

WEZI wawili sugu wa ng’ombe walipigwa na umma hadi kufa kwa madai ya kujaribu kuiba nyati katika kijiji cha Bankatti, wilaya ya Godda nchini India, Juni 13, 2018.

Gazeti la Indian Express limeripoti kwamba polisi kutoka kituo cha Deodand walitia nguvuni watu wanne waliohusika na mauaji hayo na pia watu wawili waliodaiwa kuiba nyati.

Ripoti ya polisi kutoka kituo hicho inasema kwamba wafu walikuwa na historia ndefu ya kuiba ng’ombe.Kulingana na polisi, tukio hilo lilifanyika Juni 13, 2018 katika kijiji cha Bankatti kwenye mpaka wa Deodand na Sunder Pahari wilayani Godda.

Inasemekana ‘wezi hao wa nyati’ walipatikana wakitoweka na wanyama hao kutoka kijiji kimoja. Uchunguzi zaidi unafanyiwa waathiriwa hao waliotambuliwa kama Mumtaza Ansari kutoka kijiji cha Taljhari na Charku Ansari kutoka kijiji cha Banjhi karibu na kituo cha polisi cha Poraiyahat.

You can share this post!

KWAHERI UTAPIAMLO: Majani ya viazi vitamu yanavyovutia...

Rambo achunguzwa kwa dhuluma za ngono

adminleo