• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:45 AM
Outering Road iaongoza kwa idadi ya ajali barabarani – NTSA

Outering Road iaongoza kwa idadi ya ajali barabarani – NTSA

Na BERNARDINE MUTANU

Idadi ya watu waliofariki barabarani kati ya Januari 1 na Juni 11, 2018 imefikia 1,348 kulingana na Mamlaka ya Uchukuzi na Usalama Barabarani (NTSA) Jumatano.

Eneo lililo na idadi kubwa ya waliofariki dunia katika ajali za barabarani ni Nairobi ambapo barabara ya Outering ina idadi kubwa zaidi .

Idadi kubwa zaidi ya waliofariki barabarani ni watu wanaotembea kwa miguu (515) wakilinganishwa na 497 katika kipindi kama hicho mwaka jana.

Idadi ya abiria waliofariki ni 297, wakilinganishwa na 335 katika kipindi hicho mwaka jana, ilisema NTSA, ilhali idadi ya madereva walioaga dunia ilikuwa ni 145 ikilinganishwa na 147 mwaka jana.

Walioaga dunia katika ajali za bodaboda walikuwa ni 115 wakilinganishwa na 118 mwaka wa 2017, ilisema NTSA.

Waendeshaji 25 wa baiskeli waliaga dunia katika kipindi hicho, ongezeko la asilimia 21 katika kipindi hicho mwaka jana.

Barabara ya Outering ilikuwa na asilimia ya juu zaidi ya vifo, ambapo watu 23 waliaga dunia ikilinganishwa na barabara zingine Nairobi, ilisema ripoti hiyo.

You can share this post!

Jubilee Insurance kuwapa bima Wakenya wa pato la chini

Kampeni ya kuwabamba wazee wanaooa wasichana matineja yaanza

adminleo