• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Polo akemea mke kwa kuomba chumvi kwa dume jirani

Polo akemea mke kwa kuomba chumvi kwa dume jirani

Na JOHN MUSYOKI

MAJENGO, EMBU

SINEMA ya bure ilishuhudiwa mtaani hapa kalameni mmoja alipomgombeza mkewe kwa kuomba chumvi kutoka kwa jirani.

Duru zinasema kuwa jamaa aliasi ukapera majuzi na hakutaka mkewe kushirikiana na wapangaji hasa wanaume.

Siku ya kioja, kalameni alipofika nyumbani jioni alipigwa na mshangao mkubwa kupata demu katika chumba cha barobaro mmoja akiomba chumvi na akadhani walikuwa wakipiga gumzo za hapa na pale.

Jamaa alikasirika na kujitoma ndani ya chumba na kuanza kumgombeza demu nusura amwangushie makonde akimshuku alikuwa akigawa asali.

“Wewe ni mwanamke sampuli gani? Kumbe umekuwa ukishirikiana na wanaume hapa plotini kula uroda. Leo ni leo basi msema kesho ni mwongo. Nimekupata mimi mwenyewe. Utajutia siku za kuzaliwa kwako,” kalameni alimfokea demu wake.

Mwanadada alijaribu kumweleza kwamba alikuwa akiomba chumvi lakini jamaa hakusikia la mwadhini wala la mteka maji msikitini. Aliendelea kumtetesha vikali bila kusita.

Inasemekana mwenye chumba aliamua kumsaidia mwanadada huyo kwa sababu alikuwa amezidiwa maarifa lakini juhudi zake ziliambulia patupu alipotishwa vikali.

“Unamtetea kwa nini? Kumbe umekuwa ukinyemelea mke wangu na ndio mnadai alikuwa akiomba chumvi. Wewe ni mtu bure kabisa. Utakiona cha mtema kuni,” jamaa alisema.

Wakati majamaa walipokuwa wakimenyana, demu alipata nafasi ya kuponyoka na kutoka shoti ungedhani alikuwa akifukuzwa na pepo.

Ilibidi baadhi ya wapangaji kuingililia kati na kuzima mzozo huo. Demu alikimbililia usalama wake na haikujulikana iwapo alirejea.

maa huyo tena.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

Karua bado aamini alimbwaga Waiguru, akata rufaa tena

TAHARIRI: Walaghai wasiendelee kukosesha taifa mabilioni

adminleo