• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 6:47 AM
Kuira bingwa wa Shibetsu Half Marathon

Kuira bingwa wa Shibetsu Half Marathon

Na GEOFFREY ANENE

MKENYA Paul Kuira aliibuka mshindi wa mbio za Shibetsu Half Marathon nchini Japan baada ya kuzikamilisha kwa rekodi mpya ya saa 1:03:10 Julai 22, 2018.

Kuira alilazimika kufanya kazi ya ziada katika hatua za mwisho kwenye mbio hizi za kilomita 21 zilizofanyika wakati wa joto kali na kuwanyima Wajapani Tomohiro Tanigawa na Tsubasa Hayakawa ushindi. Tanigawa alikamilisha katika nafasi ya pili kwa saa 1:03:15 naye bingwa mtetezi Hayakawa akafunga tatu-bora kwa saa 1:03:18.

Mkenya James Ndirangu alishikilia rekodi ya Shibetsu Half Marathon ya saa 1:03:22 aliyoweka akishinda taji la mwaka 2016 kabla ya Kuira kuifuta.

Kuira ni mwanamume wa tano kutoka Kenya kuwahi kushinda mbio hizi baada ya Solomon Kariuki (1996), Kipng’eno Kibet (2008), Kiragu Njuguna (2009) na Ndirangu (2016).

Wakenya Esther Wanjiru, Ruth Wanjiru na Winfrida Kebaso wamewahi kunyakua mataji ya Shibetsu Half Marathon. Esther alitawazwa bingwa mwaka 1996 na 1999, Ruth akashinda mwaka 2006 naye Kebaso akaibuka mshindi mwaka 2015. Kotomi Tsubokura alihakikisha taji la mwaka huu linasalia nchini Japan alipokata utepe kwa saa 1:15:42.

Matokeo (Julai 22, 2018):

Wanaume (Kilomita 21)

  1. Paul Kuira (Kenya) saa 1:03:10
  2. Tsubasa Hayakawa (Japan) 1:03:15
  3. Tomohiro Tanigawa (Japan) 1:03:18
  4. Ryo Matsumoto (Japan) 1:03:44
  5. Kenta Iinuma (Japan) 1:04:21

Wanawake (Kilomita 21)

  1. Kotomi Tsubokura (Japan) 1:15:42
  2. Ayaka Inoue (Japan) 1:16:15
  3. Kikuyo Tsuzaki (Japan) 1:16:22
  4. Madoka Nakano (Japan) 1:16:28
  5. Hiroko Miyauchi (Japan) 1:16:38

Wanawake (Kilomita 10)

  1. Natsuki Omori (Japan) dakika 34:08
  2. Mai Ito (Japan) 34:16
  3. Junna Suzuki (Japan) 34:17
  4. Ikumi Fukura (Japan) 34:21

5. Kanako Takemoto (Japan) 34:28

  • Tags

You can share this post!

Obiri avunja rekodi kwenye mita 5,000

Watoto 5 wabambwa kwa kubaka msichana kwa zamu

adminleo