• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Kizimbani kwa kuiba TV watazame Kombe la Dunia

Kizimbani kwa kuiba TV watazame Kombe la Dunia

Na RICHARD MUNGUTi

WASHUKIWA wawili waliompora mwenye duka la elektroniko televisheni kutazama mechi za Kombe la Dunia  walifikishwa mahakamani kujibu mashtaka. 

Mabw Alfred Oyugi Orwaru na Franc Omondi Amolo walikanusha shtaka la kupokea mali kwa njia ya udanganyifu.

Hakimu mkuu katika mahakama ya Milimani Francis Andayi alijaribu awezalo kujua sababu ya washtakiwa kutolipa mwenye duka lakini “walinyamaza kabisa.”

“Nataka mnieleze sababu hamkulipa mwenye duka televisheni aliyowapatia yenye thamani ya Sh65,000,” hakimu aliwahoji.

Akamwulia Oyugi , “Wewe nieleze ulimlipa mwene duka pesa gapi?”

Alijibu, “Nilienda  kwa Bw Robinson Murage nikamlipa pesa kisha nikapewa runinga.”

Lakini licha ya kuwashauri kuwa atawaachilia kwa vile pesa wanazodaiwa ni ndogo “hawakutoboa siri ya kukataa kulipia televisheni hiyo.”

“Sitaki kuharibu wakati na kesi ya Sh65,000. Muda uliopo ni wakuamua kesi za milioni mia tano na mabilioni ya umma yaliyoibwa. Mngeliomba msamaha ningeliwaachilia kisha niwaambie mkitaka kuendelea na wizi endeleeni tutakuja kuokota maiti zenu kama mmepigwa na raia,” Bw Andayi.

Washtakiwa waliomba wapewe muda wasuluhishe deni hilo na Bw Murage.

Kesi hiyo itatajwa Julai 23, 2018 kwa vile Bw Murage hakuwa na mtu wa kumwacha kwenye duka afike kortini kurekodi makubaliano.

You can share this post!

Wanakijiji waua mamba 300 kulipiza kisasi

Sukari sasa ni salama, Munya aambia Wakenya

adminleo