• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 4:55 PM
Kerr amtetea kipa kulambishwa mabao 2 na Yanga

Kerr amtetea kipa kulambishwa mabao 2 na Yanga

Na JOHN ASHIHUNDU

Kocha wa Gor Mahia, Dylan Kerr amemtetea kipa Boniface Oluoch anayeshutumiwa baada ya kufungwa mabao mawili katika ushindi wao wa 3-2 dhidi ya Yanga ya Tanzania kwenye mechi ya Kundi D ya michuano ya Confederations Cup.

Oluoch alilaumiwa vikali na mashabiki K’Ogalo kutokana na mabao hayo yaliyoingia kiholela mbele ya mashabiki wengi waliomiminika katika uwanja wa Kitaifa jijini Dar es Salaam.

Lakini akizungmza kuhusu mechi hiyo, Kerr alisema: “Hii ni mechi ambayo tungefunga mabao saba katika kipindi cha kwanza lakini hatukutumia nafasi nyingi tulizopata. Nimefurahia ushindi wa 3-2 kwa sababu umetuweka katika mazingara mazuri mashindanoni.” Kwa upande wa Yanga, naibu kocha, Noel Mwandila alieleza jinsi walivyochanganywa kutokana na bao la mapema.

K’Ogalo walipata bao la kwanza kupitia kwa George ‘Blackberry’ sekunde ya 38.

“Boniface alifanya kazi kubwa majuzi dhidi ya AFC Leopards kwa kuokoa hatari kubwa tulipokuwa sare, kabla ya kuibuka na ushindi wa 2-1. Nina Imani naye kwa asilimia kubwa.”

Baada ya ushindi huo, K’Ogalo’s wamechukua uongozi wa Kundi hilo baada ya USM Algers ya Algeria kutoka sarea na Rayon Sport ya Rwanda katika mechi nyingine iliyochezewa Mustapha Tchaker Stadium nchini Algeria mwishoni mwa wiki.

Baada ya kila timu kucheza mechi nne, Gor Mahia wanaongoza kwa point inane, sawa na USM, huku zote zikiwa na nafasi kubwa ya kufuzu kwa hatua ya robo-fainali. Ajabu ni kwamba, timu hizo mbili zina tofauti sawa ya mabao.

Rayon wanashikilia nafasi ya tatu wakiwa na pointi tatu nab ado wana nafasi ya kufuzu kwa robo-fainali.

Yanga wako nje ya kampeni za kuwania nafasi ya kutinga robo-fainali baada ya kujiokotea pointi moja.

Mbali na kuweka historia barani Afrika, kufuzu kwa Gor Mahia kwa hatua ya robo-fainali kutawaongezea mgao wa pesa.

Tayari mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL) wameweka mfukoni Sh27 milioni kwa kutinga hatua ya makundi na wataongezwa kitita kingine cha Sh8 milioni iwapo watafuzu kwa robo-fainali, kwa kuandikisha sare au ushindi katika mechi ijayo dhidi ya Rayon iliyopangwa kuchezwa Agosti 19, jijini Nairobi.

Timu zitakazofuzu hatua ya nusu-fainali zitapokea Sh45 milioni, huku mabingwa wa taji hilo la ligi ndogo ya bara wakipokea Sh125 milioni kutoka kwa CAF.

You can share this post!

Jericho wachupa kileleni Super 8

Wazito wasisitiza watasalia ligini

adminleo