• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 3:04 PM
Barcelona, PSG na Juventus kivumbini kumsajili Pogba

Barcelona, PSG na Juventus kivumbini kumsajili Pogba

Na MASHIRIKA

Tetesi zinadai kwamba kiungo mbunifu Paul Pogba anang’ang’aniwa na klabu za Barcelona, Paris Saint-Germain (PSG) na timu yake ya zamani Juventus.

Wakala wa Mfaransa huyu wa Manchester United anatarajiwa kuwasili uwanjani Old Trafford juma hili kwa mazungumzo muhimu kuhusu hali yake.

Vyombo vya habari nchini Uingereza vinasema Mino Raiola ataeleza United kwamba anaweza kufanikisha mpango wa uhamisho hadi Barcelona wa Sh13 bilioni.

Juventus na PSG pia zimehusishwa na nyota huyu aliyetua United kwa Sh11.6 bilioni kutoka Juventus mwaka 2016.

Maisha ya baadaye ya Pogba, 25, uwanjani Old Trafford yamekuwa ya wasiwasi kutokana na uhusiano wake na kocha mkuu Jose Mourinho kuzorota. Pogba anasalia na miaka mitatu kwenye kandarasi yake na United.

Raiola pia anawakilisha kiungo Mwitaliano Marco Verratti, ambaye wakati mmoja United ilivutiwa naye sana.

Huku kipindi kirefu cha uhamisho kikiratibiwa kufungwa Agosti 9, huenda watu wakashuhudia Pogba akielekea Barca katika mpango wa kubadilishana wachezaji utakaohusisha raia wa Colombia Yerry Mina kuhamia Old Trafford kutoka Camp Nou. United inamezea mate Mina, ambaye bei yake ni Sh4.5 bilioni.

You can share this post!

Chelsea sasa yataka usogora wa Ramsey

Lucy Wangui agunduliwa kuwa mtumizi sugu wa pufya

adminleo