• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 5:55 AM
Wanandoa wanyweshwa mkojo kwa kuoana kisiri

Wanandoa wanyweshwa mkojo kwa kuoana kisiri

Na MASHIRIKA

MADHYA PRADESH, INDIA

MWANAMUME na mke wake walitekwa nyara wakapigwa na kulazimishwa kunywa mkojo na familia ya mke huyo ambayo ilidai aliolewa bila idhini yao.

Ripoti zinasema mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 23 alifugwa kwenye mlingoti na kutandikwa huku mke wake, 21, akivuliwa nguo na kunyolewa nywele kisha wakalazimishwa kunywa mkojo.

Video iliyosambazwa mitandaoni ilionyesha kisa hicho ambacho kilithibitishwa kilitendeka katika eneo la Alirajpur, Madhya Pradesh, India.

Ilisemekana wawili hao waliishi katika kijiji kimoja ndipo wakaoana Mei mwaka huu ilhali familia ya mke ilikuwa haijaidhinisha ndoa hiyo.

Kulingana na mashirika ya habari, mwanamume huyo alijitahidi kuwaomba waruhusu waoane na hata akalipa mahari ya mbuzi wawili na pesa lakini wapi!

Iliwabidi waoane kisiri kisha wakahama kijiji hicho lakini walipoenda kutembelea jamaa zao hivi majuzi, walishikiwa bunduki na kutekwa nyara kisha wakapigwa na kuaibishwa hadharani.

Polisi walinukuliwa kusema walitekwa nyara katika nyumba ambako walikuwa wakiishi wakati huo.

Wahusika kadhaa walikamatwa kwa kuhusika katika kisa hicho.

-Imekusanywa na Valentine Obara

You can share this post!

Kocha asifu vijana wake kuandaa gozi kama alivyowaagiza

Alilamba vya pembeni, sasa hana ‘transfoma’...

adminleo