• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Vita lojing’i baada ya polo kukataa kulipia asali aliyochovya

Vita lojing’i baada ya polo kukataa kulipia asali aliyochovya

Na Leah Makena

Giaki, Meru

SINEMA ya bure ilishuhudiwa kwenye lojing’i moja eneo hili pale jombi na kimwana walipochapana jamaa alipodinda kulipia huduma za uroda.

Duru zasema kuwa wawili hao waliamua kulishana asali kwenye chumba hicho wiki moja baada ya kujuana lakini demu akataka kulipwa kwa huduma akidai polo angeingia mitini baada ya kuonja asali.

Licha ya polo kusititiza kuwa alitaka mrembo wa kuoa, kidosho alishikilia alitaka malipo.Yasemekana kuwa mambo yaliharibika jamaa alipomkabidhi kidosho noti ya shllingi mia moja badala ya shilingi mia tano walivyokuwa wamekubaliana.

Hakuamini polo alipodai alikatiza muda waliokuwa wamepanga kurushana roho kwa nia ya kuokoa uhusiano wao na pesa alizompa zilitosha.

Hapo ndipo hasira za mwanadada zilipanda na akachokoza nyuki alipojaribu kuchukua pesa kwa nguvu kutoka mfuko wa koti ya jamaa.

Vuta nikuvute ilibadilika kuwa vita zilivyofanya wengi kuacha shughuli zao ili kuwatenganisha. Hakuna aliyekubali kumshawishi polo kuongezea demu hela.

Alidai kidosho alitaka kupora pesa zake. Hatima ya mzozo huo haikujulikana kwani mrembo alishikilia kuwa alitaka haki yake jamaa alivyokuwa amemuahidi.

 

You can share this post!

Mama mkwe amnyima jombi kiti eti ana kiburi

OBARA: Kutunza mazingira ni bora kuliko ajenda zote

adminleo