• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Mwekezaji pabaya kwa kujenga jumba la Waititu bila idhini

Mwekezaji pabaya kwa kujenga jumba la Waititu bila idhini

Na RICHARD MUNGUTI

MWEKEZAJI aliyefumaniwa akijenga jumba linalohusishwa na Gavana wa Kiambu Bw Ferdinand Waititu alishtakiwa Jumatano.

Bw Robert Rukwaro alikabiliwa na shtaka la kujenga jumba bila kuidhinishwa na idara ya ujenzi ya baraza la kaunti ya Nairobi.

Bw Rukwaro alishtakiwa muda mfupi baada ya mkewe Bw Waititu , kukanusha mashtaka ya kumiliki jumba bila leseni katika kwa kaunti ya Nairobi.

Bw Rukwaro aliyekanusha shtaka la kuendelea na ujenzi bila kibali kutoka kwa idara ya mipango na ustawi wa kaunti aliomba aachiliwe kwa dhamana.

Wakili Manases Mwangi aliymwakilisha mshtakiwa aliomba pia korti iamuru upande wa mashtaka uwakabidhi nakala za kesi ndipo aandae utetezi.

Kesi itatajwa Septemba 6.

You can share this post!

Wanafunzi vyuoni kutumia kadi za kidijitali kupokea mikopo...

Swazuri ang’olewa mamlakani NLC

adminleo