• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 5:29 PM
Kesi ya tatu ya sakata NYS kuanza Februari 2019

Kesi ya tatu ya sakata NYS kuanza Februari 2019

Na RICHARD MUNGUTI

MOJA ya kesi tatu dhidi ya waliokuwa maafisa wa shirika la huduma ya  vijana kwa taifa ya sakata ya Sh469 milioni itaanza kusikizwa Februari 7, 2019.

Kesi hiyo ilitengewa siku hiyo washukiwa 44 walipofika kortini. Baadhi ya walioshtakiwa ni aliyekuwa katibu mkuu Bi Lilian Omollo , aliyekuwa mkurugenzi mkuu NYS Dkt Richard Ndubai na washukiwa wengine 41..

Kiongozi wa mashtaka Bw Gitonga Riungu alieleza Bw Ooko kuwa atatayarisha cheti kingine cha mashtaka kitakachowashirikisha washukiwa wote 47.

Faili tatu zimeunganishwa kuwa kesi moja baada ya hakimu mkuu Bw Douglas Ogoti kumwamuru Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji agawanye kesi 10 zinazowakabili washukiwa hao wanaojumuisha wafanyabiashara wa Naivasha wa Familia ya Ngirita kuwa tatu.

“Kufuatia maagizo ya Bw Ogoti nimeunganisha kesi tatu kusikizwa kwa pamoja kwa vile mashahidi ni wamoja,” alisema Bw Riungu.

Kiongozi huyo wa mashtaka alisema kuwa kuna washukiwa watatu ambao hawajajibu mashtaka.

Mawakili wanaowatetea washtakiwa wakiongozwa na wakili Migosi Ogamba walisema wamepokea nakala za mashahidi kutoka kwa afisa anayechunguza kesi hiyo.

Mahakama ilifahamishwa kuwa nakala za usahidi ambazo hazijapokewa zitachukuliwa katika afisi ya Mkurugenzi wa Jinai (DCI).

You can share this post!

EACC yapewa fursa ya mwisho kuwakamata Wakhungu na Waluke

Taabani kwa kujaribu kulaghai kampuni ya bima

adminleo