• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Maafisa wa KEBS kukaguliwa upya

Maafisa wa KEBS kukaguliwa upya

Na BERNARDINE MUTANU

Maafisa wa Shirika la Kukadiria Ubora wa Bidhaa (KEBS) watakaguliwa upya kulingana na Waziri wa Viwanda Peter Munya.

Waziri huyo Jumatano alisema kulikuwa na mipango ya kutekeleza marekebisho KEBS na kuongeza idadi ya wafanyikazi na kuwachunguza upya maafisa wa sasa.

Bw Munya alitoa agizo kwa bodi kubuni mikakati ya kuchunguza upya maafisa hao, katika zoezi litakaloanza mara moja.

“Tuna mpango wa kuongeza kiwango cha wafanyikazi, lakini tunataka kwanza kutathmini kiwango cha maadili kwa tunaowaajiri,” alisema Bw Munya.

Kulingana na waziri huyo, maafisa wa KEBS na maafisa wengine wa utekelezaji ni sehemu ya changamoto ilioko katika vita dhidi ya bidhaa ghushi na za magendo.

Maafisa wakuu wa KEBS akiwemo meneja mkurugenzi Charles Ongwae Juni walishtakiwa kwa uagizaji wa mbolea ya ubora wa chini na uenezaji wa stempu feki za KEBS.

You can share this post!

Bei ya sukari kushuka

Aliyeanika picha kujitapa anavyonajisi watoto anyakwa

adminleo