• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:23 PM
Wabunge wafika kortini kumliwaza mwenzao aliyeshtakiwa kwa ufisadi

Wabunge wafika kortini kumliwaza mwenzao aliyeshtakiwa kwa ufisadi

Na RICHARD MUNGUTI

WABUNGE watatu Alhamisi walifika katika mahakama ya kuamua kesi za ufisadi ya Milimani kumliwaza Mbunge wa Embakasi Kaskazini Bw James Gakuyu aliyeshtakiwa kwa ufisadi.

Waliofika mahakamani kumtembelea Bw Gakuyu ni pamoja na Mbunge wa Starehe Bw Charles Kanyi Njagua almaafuru Jaguar, Mbunge wa Embakasi ya Kati Bw James Mwangi na Mbunge wa Kamkunji Bw Yusuf Hassan.

Wabunge hao watatu walifika mahakamani mwendo wa saa nane mchana. Walimweleza Bw Gakuyu kwamba watamuunga mkono kwa hali na mali.

Bw Gakuyu na washukiwa wengine 11 walikana mashtaka 27 ya kufuja pesa za hazina ya kustawisha eneo bunge (CDF). Walidaiwa walipokea kinyume cha sheria Sh39 milioni.

Bw Gakuya aliachiliwa kwa dhamana ya Sh2 milioni pesa tasilimu. Washtakiwa wengine waliachiliwa kwa dhamana ya Sh1.5 milioni na wengine wakapewa dhamana ya Sh750,000.

You can share this post!

Akana kumeza mamilioni ya Dubai Bank

Gor kunufaika na Sh12m kwa mauzo ya Walusimbi

adminleo