• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 3:03 PM
Ahmednassir akaangwa na Maraga kwa kutumia lugha chafu mitandaoni

Ahmednassir akaangwa na Maraga kwa kutumia lugha chafu mitandaoni

Wakili Ahmednassir Abdullahi (kulia) akiwa katika Mahakama ya Juu . Picha/RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

MAKABALIANO makali yalitanda katika Mahakama ya Juu Ijumaa wakati Jaji Mkuu (CJ) alipomtaka wakili Ahmednassir Abdullahi aamue ikiwa atakuwa anafanya kesi katika mahakama au katika mitandao ya kijamii.

Jaji Maraga aliyekuwa anasikiza kesi ya raia wawili wa Iran wanaotakiwa kurudishwa kwao baada ya kifungo cha maisha kufutiliwa mbali na mahakama ya rufaa.

Jaji Maraga anasikiza rufaa iliyokatwa na afisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma (DPP) akiwa na Jaji Mohammed Ibrahim, Jackton Ojwang, Smokin Wanjala na Isaac Lenaola.

Kabla ya kuanza kusikiza kesi hiyo Jaji Maraga alimtaka Bw Abdullahi aeeleze matusi na lugha chafu ambayo amekuwa akitumia dhidi ya mahakama kutokana na maagizo mbali mbali,

Bw Abdullahi aliomba msamaha na kuahidi hatarudia hayo tena.

Katika siku za hivi punde amekuwa akikashifu mahakama kwa maagizo inayotoa.

You can share this post!

Blatter ataka Kombe la Dunia 2026 liandaliwe Morocco

Nani ataibwaga KCB kwenye Ligi Kuu ya Raga?

adminleo