• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Deya aachiliwa kwa dhamana ya Sh10 milioni

Deya aachiliwa kwa dhamana ya Sh10 milioni

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA  Kuu jumanne ilimwachilia Askofu Gilbert Deya kwa dhamana ya Sh10 milioni.

Jaji Luka Kimaru alisema ijapokuwa kuna tashwishi Deya atachana mbuga, ameona heri amwachilie kwa vile upande wa mashtaka ulishindwa kukamilisha kesi katika muda wa siku 90.

“Mshtakiwa huyu anashukiwa atatoroka lakini upande wa mashtaka haukukamilisha kesi dhidi yake katika muda wa siku 90 kama ilivyoamriwa na mahakama kuu miezi mitano iliyopita,” alisema  Jaji Kimaru.

Jaji alisema atamwekea masharti makali Askofu Deya anayekabiliwa na mashtaka ya kuiba watoto.

Mahakama ilisema Askofu Deya yuko na tabia ya kuikejeli mahakama na  pia kujaribu kutoroka.

Mnamo Desemba 2017 hakimu mkuu Francis Andayi alikuwa ameamuru mshtakiwa aachiliwe kwa dhamana ya Sh1 milioni.

Askofu ameshtakiwa kwa wizi wa watoto wadogo.

You can share this post!

Mhasibu akana kuiba mamilioni ya mwajiri

Washukiwa wengine 3 wakodolea macho kifo

adminleo