• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Esperance ya Tunisia yatua nchini kuchuana na Gor Machakos

Esperance ya Tunisia yatua nchini kuchuana na Gor Machakos

Na GEOFFREY ANENE

MIAMBA wa soka wa Tunisia, Esperance, wamewasili nchini Kenya kwa mchuano wa mkondo wa kwanza wa raundi ya kwanza ya Klabu Bingwa Afrika.

Mabingwa hawa wa Tunisia mara 27 wametua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Jumatatu usiku.

Esperance, ambao walishinda mataji ya Afrika mwaka 1992 na 2017 na kumaliza nambari mbili mwaka 1999, 2000, 2010 na 2012, watalimana na wenyeji Gor Mahia hapo Machi 7 saa kumi jioni uwanjani Kenyatta mjini Machakos.

Mabingwa mara 16 wa Kenya, Gor, hawajawahi kushinda mashindano haya ya kifahari katika historia yao.

Gor ya kocha Dylan Kerr iliwahi kukutana na Esperance katika ulingo wa kimataifa kwenye shindano la Cup Winners’ Cup mwaka 1987. Ilinyakua taji kwa mabao ya ugenini baada ya sare ya 2-2 jijini Tunis nchini Tunisia na 1-1 jijini Nairobi. 

Gor ilinyakua tiketi ya kushiriki raundi ya kwanza ilipobandua nje Leones Vegetarianos ya Equatorial Guinea kwa jumla ya mabao 3-1 nayo Esperance ikang’oa ASAC Concorde ya Mauritania mashindanoni kwa jumla ya mabao 6-1.

You can share this post!

Kazi rahisi kwa Prisons na Pipeline baada ya droo ya...

Kimetto kushiriki Boston Marathon baada ya miaka minne

adminleo