• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 6:55 AM
Faxe Gold, bia mpya yatua mitaani kushindana na Tusker

Faxe Gold, bia mpya yatua mitaani kushindana na Tusker

Na BERNARDINE MUTANU

Kampuni ya kutengeneza pombe ya Demark, Royal Unibrew imezindua mauzo ya bia mpya nchini Kenya.

Kampuni hiyo ilizindua pombe Faxe Gold ambayo itashindana na aina za pombe zilizoko nchini zenye uwezo wa kiwango cha wastani kama Tusker, Pilsner, White Cap na Allsops.

Kiwango cha pombe kilichoko ndani ya kileo hicho ni asilimia 5.5 na itapatikana ndani ya chupa ya milimita 330 na chupa za milimita 500.

Tayari, kuna pombe Faxe 10 na Faxe Stout 7.7 nchini Kenya.

Faxe Gold itasambazwa na Patiala Distillers, na inatarajiwa kushindana na pombe zingine nchini zenye uwezo huo.

You can share this post!

Jamii zilizobaguliwa kunufaika na sera ya kugawa rasilimali

Kundi la wenye magari kuwapa chakula wakazi wa pato la chini

adminleo