• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:25 PM
GUMZO: Arsenal inamtaka beki wa Dortmund

GUMZO: Arsenal inamtaka beki wa Dortmund

IMEKUSANYWA NA CECIL ODONGO

YAPO madai kuwa Arsenal inapanga kumsajili beki wa kati wa Dortmund Manuel Akanji ambaye aling’aa sana msimu uliopita.

Raia huyo wa Uswisi aliye na umri wa miaka 26 alishiriki karibu mechi zote za Dortmund msimu uliopita akiisaidia kumaliza katika nafasi ya pili kwenye Bundesliga.

Dortmund wapo tayari kuachilia Akanji baada ya kusajili Niklas Sule na Nico Schlotterbeck na pia kufutwa kwa kocha Marco Rose aliyependa sana kumchezesha.

Hata hivyo, changamoto ni kuwa Arsenal inamsaka beki ambaye anatumia sana mguu wa kushoto wa kumsaidia Gabriel Magalhaes ilhali Akanji anatumia ule wa kulia.

Pia Arsenal inaoenekana kuwa na mabeki wa kutosha kwa sababu William Saliba atakuwa akirejea kutoka Marsaille ambako amekuwa akicheza kwa mkopo na pia wapo Ben White na Rob Holding.Iwapo atatua Arsenal ataungana na raia mwenzake Granit Xhaka anayewajibikia The Gunners.

  • Tags

You can share this post!

DOUGLAS MUTUA: Amerika, China zisisukume mataifa mengine...

TZ yawarai viongozi wa upinzani walio uhamishoni warejee

T L