• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Kesi 5 za wizi benki ya Equity kuunganishwa

Kesi 5 za wizi benki ya Equity kuunganishwa

Na RICHARD MUNGUTI

MKURUGENZI wa mashtaka ya umma (DPP) Bw Noordin Haji atajumuisha kesi tano dhidi ya wafanyakazi wa benki ya Equity wanaoshtakiwa kwa wizi wa mamilioni ya pesa.

Hakimu mkazi Hellen Onkwani alimwamuru Bw Noordin awasilishe ombi hilo mnamo Aprili 30 kesi hizo zitakapotajwa.

Kiongozi wa mashtaka Bi Addah Sega alimweleza hakimu kwamba anasubiri maagizo kutoka kwa Noordin kuhusu kuunganishwa kwa kesi hizo.

Bi Sega alisema hayo baada ya mfanya kazi mwingine wa benki hiyo Fredrick Kitaka Muoki  aliposhtakiwa kwa wizi wa Sh3.4milioni.

Wengine watakaoshtakiwa pamoja na Muoki ni  James Omoto Otembo na Stephen Wanjii Githinji.

James na Stephen wanakabiliwa na shtaka la wizi wa Sh 4.6 milioni kila mmoja kutoka kwa benki ya Equity.

Wakop nje kwa dhamana ya Sh300,000 pesa taslimu.

You can share this post!

Kenya yalazimishwa sare tasa na Ethiopia U-17

SHAIRI: Ukihitaji habari, tafuta Taifa Leo

adminleo