• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 6:27 PM
Mama, 75, ashinda kesi ya kufurusha wanawe wa kiume wasiochangia hata kitunguu licha ya kufanya kazi

Mama, 75, ashinda kesi ya kufurusha wanawe wa kiume wasiochangia hata kitunguu licha ya kufanya kazi

NA MASHIRIKA

PAVIA, ITALIA

MWANAMKE mmoja nchini Italia amechukua hatua ya kisheria kuwatimua wanawe wawili wa kiume wenye umri wa miaka 40 na 42 ambao walikuwa wamekatalia kwa nyumba yake licha ya kufanya kazi.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka,75, kutoka mji wa kaskazini wa Pavia, alichoshwa na uzembe wa wanawe hao licha ya kuwarai mara kwa mara watafute makao na wawe watu wa kujitegemea baada ya kupata ajira.

“Hakuna yeyote kati ya wanangu hawa wawili aliyetaka kujua,” mama alisema, kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa kwenye gazeti la La Provincia Pavese.

Mama huyo alilazimika kuelekea mahakamani akilalama kwamba watoto hao hawakuwa wakimsaidia kununua hata kitunguu nyumbani.

Vile vile, walimuachia kazi zote za nyumbani licha ya umri wake kusonga.

Jaji wa Pavia, Simona Caterbi, aliisikiliza kesi hiyo na kutoa uamuzi kwamba watoto hao watu wazima almaarufu Bamboccioni watimuliwe nyumbani.

  • Tags

You can share this post!

Songombingo Marereni walimu wa bodi wakiandamana kudai...

Ex wa Diamond Hamisa Mobetto kufanya kazi na hasimu wa...

T L