Na MWANGI MUIRURI
Mnamo Agosti 10, Seneta matata Bi Karen Nyamu alijitokeza akiombea Man United msimu mbaya wa 2023/24 na kwa sasa, ni kama imani yake iko sawa.
Baada ya Man U kufungua msimu kwa kupata pointi tatu baada kwa kuadhibu Wolves 1-0, Bi Nyamu alikuwa mwenye tabasamu kama ya tasa aliyepata mwana baada ya Tottenham Hotspur kuikomoa Man U 2-0 mnamo Jumamosi.
“Katika michuano yote 38 ya Man U katika ligi kuu ya Uingereza, Mimi nitakuwa mpinzani wao kwa mara zote hizo,” akasema.
Alisema kwamba ikiwezekana, raha yake ni Man U washushwe daraja.
“Mimi kama mfuasi sugu wa Arsenal naapa ya kwamba nitakuwa muaminifu kama mpinzani wa Man United kwa siku zote zile…matumaini yangu yakiwa hii timu itakuwa na msimu wa kusikitisha.
Katika msimu wa 2022/23, Arsenal ilimaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Man City huku Man United wakimaliza katika nafasi ya tatu.