• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Maombi mabaya ya Karen Nyamu dhidi ya Man U yaonekana kujibiwa

Maombi mabaya ya Karen Nyamu dhidi ya Man U yaonekana kujibiwa

Na MWANGI MUIRURI

Mnamo Agosti 10, Seneta matata Bi Karen Nyamu alijitokeza akiombea Man United msimu mbaya wa 2023/24 na kwa sasa, ni kama imani yake iko sawa.

Baada ya Man U kufungua msimu kwa kupata pointi tatu baada kwa kuadhibu Wolves 1-0, Bi Nyamu alikuwa mwenye tabasamu kama ya tasa aliyepata mwana baada ya Tottenham Hotspur kuikomoa Man U 2-0 mnamo Jumamosi.

Bi Nyamu alikuwa amesema kwamba katika kila mchuano ambapo Man U itakuwa ikivaana, atakuwa akishabikia wapinzani wa vijana hao wa Erik Ten Hag.

“Katika michuano yote 38 ya Man U katika ligi kuu ya Uingereza, Mimi nitakuwa mpinzani wao kwa mara zote hizo,” akasema.

Alisema kwamba ikiwezekana, raha yake ni Man U washushwe daraja.

“Mimi kama mfuasi sugu wa Arsenal naapa ya kwamba nitakuwa muaminifu kama mpinzani wa Man United kwa siku zote zile…matumaini yangu yakiwa hii timu itakuwa na msimu wa kusikitisha.

Katika msimu wa 2022/23, Arsenal ilimaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Man City huku Man United wakimaliza katika nafasi ya tatu.

 Mnamo Septemba 3, 2023 Man U itashuka ugani kuvaana na Arsenal na ndio itasubiriwa kuonwa iwapo maombi ya Bi Nyamu yataendelea kuwa na mashiko au kudunishwa.
  • Tags

You can share this post!

YANAYOJIRI: Serikali yajiandaa kuzindua mradi wa mafuta ya...

Faini ya Sh850,000 kwa kufichua hali ya HIV ya mwenzake...

T L