• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 10:10 AM
Mpenzi aliniacha kwa kumtamani rafikiye; nishauri sababu bado nampenda

Mpenzi aliniacha kwa kumtamani rafikiye; nishauri sababu bado nampenda

Mpenzi wangu aliniacha alipogundua nilikuwa namtaka rafiki yake. Nampenda sana na ninajuta kwa kumkosea. Natamani turudiane lakini sijui kama atakubali. Nahitaji ushauri wako.

Haitakuwa rahisi kumshawishi mwanamke huyo kwa sababu kitendo chako kilithibitisha kuwa wewe si mtu wa kuaminika. Lakini unaweza kujaribu bahati yako uone kama atakusamehe.

Hataki nikiongea na mwanaume mwingine, tunakosana kila mara

Nina miaka 30 na nina mpenzi. Pia nina wanaume wengi marafiki na wengine tunafanya kazi pamoja. Lakini mpenzi wangu hapendi kuona nikizungumza na mwanamume mwingine na tunagombana kila mara kuhusu jambo hilo. Nifanye nini?

Mapenzi yana wivu. Mpenzi wako anahofia unaweza kunyakuliwa na mwanamume mwingine. Jaribu kumwelewa na uendelee kumhakikishia kuwa huna mwingine isipokuwa yeye. Hatimaye atazoea.

Shida mke wangu hajui usafi, nipe ushauri wako

Nimekuwa na mpenzi kwa miaka miwili. Nampenda kwa dhati na ningependa sana awe mke wangu. Shida yake ni kuwa hajui usafi. Nifanye nini?

Ni aibu kwa mtu mzima kuwa mchafu na zaidi kwa mwanamke. Itakuwa changamoto kubwa kwako kuishi naye. Kama anatosha mambo mengine yote kuwa mke wako, tafuta namna ya kuzungumza naye ili arekebishe upande huo.

Niliyepata mtoto naye ameoa mwingine kisha akaniahidi kunisaidia

Nina mpenzi na tumezaa mtoto. Alikuwa ameahidi kunioa lakini amebadili nia. Ameamua kuoa mwingine na ameniomba nimruhusu akiahidi kuwa ataendelea kunisaidia kulea mtoto wetu. Naomba ushauri wako.

Ingawa mpenzi wako amekuomba ruhusa, ukweli ni kuwa ameamua na huwezi kumzuia. Kubali uamuzi wake na uweke matumaini kuwa atatimiza ahadi ya msaada wa kulea mtoto.

  • Imeandaliwa na Fatuma Bariki
  • Tags

You can share this post!

Mbunge atuza watoto zawadi ya ‘kipekee’

Kilio cha familia ya kijana aliyetoweka alipoenda...

T L