• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 AM
Salat aingia Kenya Kwanza rasmi

Salat aingia Kenya Kwanza rasmi

NA VITALIS KIMUTAI

KATIBU Mkuu wa Kanu, Nick Salat ameutema muungano wa Azimio la Umoja na kujiunga na kambi ya Rais William Ruto ya Kenya Kwanza.

Bw Salat alitangaza kuwa amekata kauli ya kumuunga mkono Dkt Ruto na serikali yake kushinda uchaguzi mkuu uliopita.

Hata hivyo, hakufafanua iwapo kwa kufanya hivyo ametema chama cha Kanu kinachoongozwa na mwenyekiti aliyekuwa Seneta wa Baringo Gideon Moi.

“Ninataka kukuhakikishia kuwa nimekuunga mkono kikamilifu. Siwezi kustahimili kuwa nje ya serikali, kuwa kando na walio wengi. Nimerejea kwenye kundi,” alisema Bw Salat.

Bw Salat alikuwa anazungumza katika uwanja wa Bomet Green ambapo Dkt Ruto, Naibu Rais Rigathi Gachagua na viongozi wengine walihudhuria warsha ya maombi ya kutoa shukran.

“Kama mtoto mpotevu, ninataka kutangaza hadharani kuwa nitakuunga mkono kwa urais kwa miaka 10 ijayo,” alisema.

Bw Salat alisema japo alimuunga mkono aliyekuwa waziri mkuu, Raila Odinga kwa urais, alikubali matokeo ya urais na kumtambua Dkt Ruto kama rais wa tano wa Kenya.

  • Tags

You can share this post!

MWALIMU WA WIKI: Mwalimu anafaa kuteka saikolojia ya...

Polisi wazidisha uchunguzi kuhusu mauaji ya Chiloba

T L