• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Teranga Lions, Atlas Lions na Super Eagles mavizioni kufuzu AFCON

Teranga Lions, Atlas Lions na Super Eagles mavizioni kufuzu AFCON

NA MASHIRIKA

MABINGWA watetezi Senegal pamoja na Morocco, Mali, Algeria, Burkina Faso na Nigeria watafukuzia ushindi wa tatu mfululizo leo ili kujiweka pazuri kufuzu kushiriki Kombe la Afrika (AFCON) 2024.

Teranga Lions ya Senegal iliyopepeta Benin na Rwanda, inaalika Msumbiji mjini Diamniadio.

Vijana wa Aliou Cisse wana rekodi ya nzuri baada ya kushinda Msumbiji mara tano mfululizo.Licha ya kusikitisha Bayern Munich, mwanasoka bora Afrika Sadio Mane anatarajiwa kuwa mmoja wa miba dhidi ya Msumbiji katika Kundi L.

Atlas Lions ya Morocco iko ugenini kuzichapa dhidi ya Afrika Kusini katika Kundi K.

Wamoroko waling’ata Bafana Bafana 2-1 kupitia mabao ya Youssef En Nesyri na Ayoub El Kaabi mwaka 2022.

Macho yatakuwa kwa ‘muuaji’ Victor Osimhen kutoka klabu ya Napoli wakati Super Eagles ya Nigeria itaalika Guinea-Bissau katika Kundi A mjini Abuja.

Mvamizi wa Liverpool, Mohamed Salah atatumai kuongoza Misri kufufua matumaini kutoka mkiani mwa Kundi D. Mafirauni wako nyumbani dhidi ya Malawi.

Aidha, mabingwa wa dunia Argentina watavaana na Panama, Australia wakabane koo na Ecuador, Japan wamenyane na Uruguay na Korea Kusini dhidi ya Colombia katika baadhi ya mechi moto za kirafiki, leo.

Ratiba ya kufuzu AFCON 2024:

Leo – Algeria v Niger, DR Congo v Mauritania, Uganda v Tanzania, Cape Verde v Eswatini, Ivory Coast v Comoros, Nigeria v Guinea-Bissau, Afrika Kusini v Liberia, Misri v Malawi, Equatorial Guinea v Botswana, Mali v Gambia, Senegal v Msumbiji, Burkina Faso v Togo, Cameroon v Namibia, Tunisia v Libya, Guinea v Ethiopia

  • Tags

You can share this post!

Ufaransa, Ubelgiji mizanini Euro 2024

Pasta anayehusishwa na vifo vya watoto akana mashtaka

T L