• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Ubelgiji bila De Bruyne na Lukaku yakomoa Belarus 8-0

Ubelgiji bila De Bruyne na Lukaku yakomoa Belarus 8-0

Na MASHIRIKA

MSHAMBULIAJI Leandro Trossard wa Brighton na Dennis Praet wa Leicester walifunga mabao yao ya kwanza ndani ya jezi za Ubelgiji na kusaidia timu hiyo ya taifa kupepeta Belarus 8-0 katika mechi ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia za 2022.

Michy Batshuayi alifungulia Uhispania karamu ya mabao katika dakika ya 14 kabla ya Hans Vanaken kufanya mambo kuwa 2-0 kwa upande wa Ubelgiji wanaoshikilia nafasi ya kwanza duniani kwa mujibu wa orodha ya Shirikisho la Soka Kimataifa (FIFA).

Trossard alifunga goli la tatu la Ubelgiji katika dakika ya 38, dakika nne pekee kabla ya Jeremy Doku kuongeza la nne.

Praet alipachika wavuni goli la tano kunako dakika ya 49 kabla ya mengine kufumwa wavuni na Christian Benteke, Trossard na Vanaken mwishoni mwa kipindi cha pili.

Matokeo hayo yaliwapaisha Ubelgiji hadi kileleni mwa Kundi E kwa alama saba kutokana na mechi tatu.

Jamhuri ya Czech walioanza kampeni zao za siku wakidhibiti kilele cha Kundi E, walishuka hadi nafasi ya pili mwishowe baada ya kuzidiwa maarifa na Wales.

Chini ya kocha Roberto Martinez, Ubelgiji walicheza mechi yao ya tatu kundini dhidi ya Belarus bila ya huduma za wanasoka matata Kevin de Bruyne na Romelu Lukaku waliopangwa kwenye benchi.

Maarifa ya wawili hao hayakuhitajika ikizingatiwa kwamba Ubelgiji walipachika wavuni jumla ya mabao matano chini ya kipindi cha dakika 50 za kwanza za mchezo.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Japan waponda Mongolia 14-0 katika mechi ya kufuzu fainali...

Uholanzi yapepeta Gibraltar bila huruma katika gozi la...