• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 6:55 PM
Visa 103 vya maambukizi mapya ya virusi vya corona vyaripotiwa katika EPL

Visa 103 vya maambukizi mapya ya virusi vya corona vyaripotiwa katika EPL

Na MASHIRIKA

JUMLA ya wanasoka na wafanyakazi 103 wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) wamepatikana na virusi vya corona chini ya kipindi cha siku saba ikiwemo Disemba 26, 2021.

Hiyo ndiyo idadi ya juu zaidi ya visa vya maambukizi mapya ya virusi vya corona kuwahi kuripotiwa katika EPL.

Idadi ya juu zaidi iliyowahi kurekodiwa hapo awali kutokana na vipimo vya kila wiki ni visa 90 vilivyoripotiwa wiki moja iliyopita.

Jumla ya vipimo 15,186 vilifanywa kati ya Disemba 20-26, 2021 tangu vinara wa EPL waanzishe mpango wa kupima wachezaji na wafanyakazi katika Ligi Kuu ya Uingereza kila siku.

Mechi 15 za EPL zimeahirishwa kufikia sasa katika mwezi huu wa Disemba kwa sababu ya msambao wa virusi vya corona.

Mnamo Disemba 20, vikosi vya EPL na klabu za Ligi za Daraja za chini katika soka ya Uingereza ziliafikiana kutandaza mechi zote za kabla ya Mwaka Mpya wa 2022 jinsi zilivyoratibiwa licha ya baadhi ya michuano kuvurugwa na corona.

Washiriki wote 20 wa kipute cha EPL walikutana wiki iliyopita kujadili jinsi mechi zote zilizoahirishwa kufikia sasa kwenye kampeni za msimu huu wa 2021-22 zitakavyoratibiwa upya.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Taharuki Farmajo akidai kumfuta kazi Waziri Mkuu Somalia

Huzuni mkazi wa Witeithie akiuawa na fisi

T L