Na WANGU KANURI
WAZIRI Msaidizi wa Uchukuzi Bi Wavinya Ndeti amejiuzulu ili ajitose rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha ugavana katika Kaunti ya Machakos.
Akizungumza na wanahabari Ijumaa, Bi Ndeti amesema kuwa anaelewa changamoto ambazo watu wa Machakos wamekuwa wakipitia ndiposa lengo lake ni kuhakikisha kuwa Machakos imeimarika kwa uongozi na kiuchumi.
“Maono yangu ni kuwawezesha watu katika kaunti ya Machakos kutumia rasilimali asili na za kubuni kikamilifu katika eneo hilo,” akasema.
Vile vile, Bi Ndeti amemshukuru Rais Uhuru Kenyatta kwa kumpa fursa kuwatumikia Wakenya na kuwasaidia kupata huduma bora za uchukuzi.