• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Zapata ajipiga kifua Ingwe itaitafuna Gor Jumapili

Zapata ajipiga kifua Ingwe itaitafuna Gor Jumapili

Na CECIL ODONGO

Mjadala wa nani jabali wa soka  nchini kati ya Klabu za GorMahia na AFC Leopard umeibuka tena baada ya kocha wa ingwe Rodoflo Zapata kujishaua kwamba wao ndio bora kuliko wapinzani wao huku kivumbi kikali cha ‘debi ya Mashemeji’ ikinukia Jumapili ijayo.

Klabu hizo mbili zenye historia ndefu ya uhasama wa tangu jadi zitavaana katika uwanja wa Kasarani kwenye mechi  kali inayosubiriwa kwa hamu na hamumu na maelfu ya mashabiki wa soka nchini.

Japo ligi ya KPL  mkondo wa pili wa Kpl unaendelea, mechi hiyo itakuwa ya mkondo wa kwanza baada ya kuahirishwa mara mbili tangu mwezi Aprili mwaka 2017..

Ingawa ilipangwa awali kusakatwa katika uwanja wa Bukhungu mjini Kakamega, AFC Leopards walilazimika kuihamisha hadi uwanja wa Kasarani ili iwe rahisi kudhibiti idadi kubwa ya mashabiki watakaojitokeza.

Matamshi ya mkufunzi huyo huenda yakazua hisia kali miongoni mwa mashabiki wa Gor na Ingwe. GorMahia ni mabingwa mara 16 wa KPL huku AFC Leopards  wanaojishaua wakipigwa kumbo na uhalisia wa mambo kwa kuwa walitwaa ubingwa mara ya mwisho mwaka wa 1998.

Kocha huyo raia wa Argentina atakuwa anasimamia debi yake ya kwanza kati ya mibabe hao na ameeleza waziwazi kwamba anapania kuishinda GorMahia ili kuwaongezea shinikizo uongozini mwa ligi.

“Ingwe ndiyo klabu kubwa zaidi nchini. Napenda presha na shinikizo za kujenga timu itakayofanya kweli na kutokemeza mbali ukame wa miaka 20 wa taji ya KPL,”  akasema Zapata

Bw Zapata aliweka wazi kwamba  lengo lake  kuu la  kutinga kati ya nafasi tatu bora za juu ligi ikakimilika.

Pia anatazamia kuweka mpango mahusi wa muda mrefu ili kusaidi Ingwe kufikia ufanisi wa juu.

Ingwe wanashikilia nafasi ya nne katika msimamo wa jedwali la ligi kwa alama 35 huku wapinzani wao GorMahia wakiselelea uongozini kwa alama 49.

You can share this post!

Wanaounga mkono Ruto Pwani waonywa

Weledi wa Mwalala utaifaa Bandari ligini – Obungu

adminleo